IQNA

Mashindano ya Qur'ani

Washindani Wawasili Misri kwa Mashindano ya Qur'ani ya Port Said

20:15 - February 02, 2024
Habari ID: 3478293
IQNA-Toleo la 7 la tukio la kimataifa la Qur'ani linatarajiwa kufanyika Port Said, kaskazini mwa Misri, Februari 2-6.

Kulingana na Gavana wa Port Said Adel Mohamed Ibrahim Yousef Al Ghadhban, washiriki katika toleo hili wanatoka nchi 50.

Alisema juhudi zimefanywa ili kutoa huduma na suhula zote muhimu kwa washiriki.

Adil Muslihi, mkurugenzi mtendaji wa mashindano hayo, alisema washindani hao wamepewa malazi katika hoteli kuu za jiji.

Mashindano hayo yameandaliwa katika kitengo cha kuhifadhi Qur'ani Tukufu kwa msaada wa Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly.

Toleo la mwaka huu limepewa jina la qari maarufu wa Misri Sheikh Shahat Muhammad Anwar (1950-2008).

/3487043

Habari zinazohusiana
captcha