IQNA

Rais Rouhani amuenzi msichana wa miaka 8 aliyehifadhi Qur'ani

6:57 - March 15, 2015
Habari ID: 2985092
Tehran (IQNA)-Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemtunuku zawadi msichana Muirani mwenye umri wa miaka 8 aliyehifadhi kikamilifu Qur'ani Tukufu.

Katika mkutano wake na, Hannanah Khalfi mwenye umri wa miaka minane na aliyehifadhi kikamilifu Qur'ani Tukufu, Rais  Rouhani alibainisha furaha yake kutokana na uwezo wa msichana huyo. Rais Rouhani alisema ni jambo la fahari kuona  familia zenye watoto wanaofungamana na Qur'ani Tukufu nchini. Huku akiitaja familia kama hiyo kuwa ni kigezo, Rais Rouhani ametoa wito wa kuimarishwa uenezwaji wa utamaduni wa Qur'ani nchini. Huku akimpongeza msichana huyo aliyehifadhi Qur'ani Tukufu, Rais Rouhani amesema: "Msichana huyu mwenye umri wa miaka minane anasoma Qur'ani kwa lahni nzuri huku akizingatia kanuni za tajwidi."

Katika mkutano huo Rais Rouhani ameitunuku zawadi ya gari familia ya msichana huyo ambaye pia ana ndugu zake wengine watatu waliohifadhi Qur'ani Tukufu kikamilifu. Katika miaka ya hivi karibuni nchini Iran kumeongezeka  idadi ya watoto wenye umri wa chini ambao wamehifadhi

Qur'ani Tukufu.../mh

2980869

captcha