Ajvatovica ni sherehe kubwa zaidi ya Kiislamu barani Ulaya na imefanyika wiki iliyopita karibu na eneo la Prusac, nchini Bosnia na Herzegovina. Sherehe hiyo imepewa jina la Ajvaz-dedo, mzee mcha Mungu aliyeikuwa na mchango mkubwa katika kueneza Uislamu eneo hilo.
Sherehe hiyo ya siku saba ilihudhuriwa na idadi kubwa ya Waislamu ambao hushiriki pamoja katika swala za jamaa.