Sheikh Shawki Allam amebainisha masikitiko yake kuwa Fatwa kama hizo husababisha matatizo kama vile mauaji na uharibifu.
Ameongeza kuwa , kuna wakati mmoja ambapo ufahamu usio sahihi wa Qur'ani Tukufu ulipelekea Misri kupotea mkondo. Amesema makundi ya kigaidi hayajaweza kufahamu maana halisi ya aya za Qur'ani na Hadithi za Mtume Muhammad SAW.
Sheikh Allam amebainisha masikitiko yake kuwa, Fatwa kama hizo potovu zimepelekea sura nzuri ya Uislamu kuharibika duniani.