Kozi hiyo fupi ya mafunzo ya Qur'an ilifanyika kwa muda wa siku 50 na kusimamiwa na Jumuiya ya Kimataifa ya Kuhifadhi Qur'an kwa kushirikiana
na kituo cha mafunzo ya kuhifadhi na kusoma Qur'an cha Sa'd ibn Mu'adh.
Mwishoni mwa duru hiyo, kulifanyika hafla kubwa
iliyohudhuriwa na walimu na wasomi wa dini ya Kiislamu wanaojihusisha na
shughuli za kufundisha kitabu hicho cha Mwenyezi Mungu, ambapo pia
washiriki walipewa zawadi mbalimbali.
Msemaji wa kozi hiyo hiyo sambamba na
kusisitizia umuhimu wa kufundishwa watoto Qur'an Tukufu, alitoa
shukurani za dhati kwa jitihada za Jumuiya ya Kimataifa ya Kuhifadhi Qur'ani katika kueneza utamaduni wa Qur'ani kote duniani. Visiwa vya Comoro ambavyo pia vinajulikana kama Ngazija vinapatikana eneo la kusini mashariki
mwa bara la Afrika katika Bahari ya Hindi. Nchi hiyo ni mwanachama wa Jumuiya ya nchi za Kiarabu
Arab League na pia Jumuiya ya Ushirikiano wa Nchi za Kiislamu OIC.
3486617