Mwandishi wa IQNA nchini Uinereza amenukuu mtandao wa QuranFocus kwamba mashindano ya 19 ya Qur'ani Tukufu yatafanyika Jumapili tarehe 7 Septemba katika kitengo cha hifdhi ya Qur'ani Tukufu.
Taasisi ya Kiislamu ya al Birr ndiyo itakayokuwa mwenyeji wa mashindano hayo ambayo lengo lake ni kuwahamasisha vijana wa Kiislamu wa Uingereza kuhifadhi Qur'ani Tukufu.
Washindi katika mashindano hayo watatunukiwa zawadi za hadi pauni elfu 5 na shahada ya kushiriki kwenye zoezi hilo.
Mashindano hayo yatawashirikisha vijana wenye umri wa chini ya miaka 22.