IQNA

Mfumo wa kifedha wa Kiislamu

Waziri Mkuu wa Ethiopia apokea Tuzo ya Kimataifa ya Mfumo wa Kifedha wa Kiislamu

13:50 - September 17, 2022
Habari ID: 3475796
TEHRAN (IQNA)-Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed amepokea Tuzo ya 2022 ya Mfumo wa Kifedha wa Kiislamu ya Kimataifa kwa juhudi zilizofanywa katika kurekebisha sekta ya fedha ya Ethiopia na kuifanya iwe jumuishi.

Katika hafla iliyofanyika Djibouti mnamo Septemba 14, 2022, Waziri Mkuu Abiy Ahmed alisema wakati wa hotuba yake kwamba "katika miaka minne pekee iliyopita, sekta ya benki ya Ethiopia ilikaribia kuongezeka maradufu katika suala la jumla ya mali, amana, mikopo na ufikiaji wa matawi.

Alisema kuwa mali za benki sasa ni zaidi ya trilioni 2 za Ethiopian Birr, zinazokua kwa wastani wa 25% kila mwaka. Marekebisho ya sera yalitengeneza mazingira mazuri ya udhibiti wa uundaji wa benki zisizo na riba na madirisha ya Kiislamu katika takriban Benki zetu zote za kawaida na taasisi za kifedha kote Ethiopia.

Matokeo yake, soko la benki lisilo na riba la Ethiopia sasa sio tu la ushindani lakini linastawi likiwa na karibu wateja milioni 14 na linakua, kulingana na Abiy Ahmed. Alisisitiza zaidi kwamba Ethiopia imejitolea kufungua sekta ya benki kwa uwekezaji wa kigeni.

4085896

captcha