Msikiti huo uko katika eneo la Caderga baina ya miji ya Gumushane na Trabzon. Msikiti huo una minara miwili mirefu na pia kuta zenye urefu wa mita 1.5 lakini la kushangaza ni kuwa hauna paa. Msikiti huo ulijengwa miaka 560 iliyopita na huwa na mjumuiko mkubwa wa waumini wakati wa Sala ya Ijumaa.