IQNA

Misahafu ya kale katika maonyesho UAE

21:19 - May 23, 2021
Habari ID: 3473938
TEHRAN (IQNA)- Misahafu 40 nadra na ya kale imewekwa katika maonyesho katika Maktaba ya Umma ya Kalba katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).

Kwa mujibu wa taarifa Misahafu hiyo inaonyesha anua ya mitindo ya kaligrafia na sanaa zinginezo za Qur’ani kama vile Tadhib hasa zilizotumika wakati wa watawala wa zama za Uthmaniya.

Misahafu hiyo inamilikiwa na mwanakaligrafia maarufu wa UAE ambaye pia amezindua warsha ya kaligrafia katika maktaba hiyo.

Halikadhalika hutoa mafunzo ya namna ya kuandika aya za Qur’ani kwa mtindo ulio katika Misahafu ya kale.  Amesema kuwa kuandaa maonyesho kama hayo kunawahimiza Waislamu kutunza Misahafu ya kale.

3973118

Kishikizo: uae nalaka misahafu
captcha